"Misri na Harakati ya kutofungamana kwa upande wowote "

"Misri na Harakati ya kutofungamana kwa  upande wowote "

Imefasiriwa na / Fatma Mahmoud


Harakati isiyofungamana upande wowote ilianzishwa na nchi zilizohudhuria Mkutano wa Bandung mnamo mwaka 1955 , na harakati hiyo ni matokeo ya vita kati ya pande hizo mbili (upande wa Ulaya , ukiongozwa na Marekani  ambayo inajumuisha NATO) , ( na kambi ya mashariki, inayoongozwa na Umoja wa Kisovyeti, ambayo inajumuisha Warsaw Pact).

Misri inazingatiwa kuwa miongoni mwa nchi muhimu zaidi  zilizoanzisha   Harakati  isiyofungamana kwa  upande wowote, ambapo  ina jukumu lake muhimu linalosifika kwa  kuanzisha, kuunda na kuendeleza harakati hiyo, na katika kukuza kuwepo kwake  na mwendelezo wake kutokana na umuhimu wake mkubwa wa kikanda na kimataifa  kwa kuzingatiwa  kuwa  inajumuisha karibu na  theluthi mbili ya nchi  ulimwenguni  zilizo wanachama katika Umoja wa Mataifa , vilevile  inazingatiwa ni upande muhimu na mpana zaidi  wa kuratibu misimamo ya nchi zinazoendelea kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa, kiuchumi na kijamii  yanayotolewa  katika ajenda ya kimataifa. Rais wa Misri Gamal Abdel Nasser anachukuliwa kuwa mmoja wa waanzilishi wa  harakati hiyo pamoja na Waziri Mkuu wa India Jawaharlal, Rais wa Yugoslavia Tito, na Rais wa Indonesia Ahmed Sukarno,    na harakati  hiyo inalenga kudumisha amani na usalama ulimwenguni na kukomesha Ukoloni kwa kiasi kikubwa , kutekeleza Uadilifu  baina ya nchi ,kuheshimu kwa wanachama wote, kukuza maslahi ya pamoja, na kuheshimu haki za binadamu.

Misri ilikuwa na mchango wa wazi katika kubadilisha mawazo yanayohusiana na kutofungamana kwa upande wowote kuwa ukweli unaoonekana katika hali halisi wakati wa kuanzishwa kwa harakati hiyo . pia imekaribisha mkutano wa kilele wake wa pili   mnamo mwaka 1964 , na mkutano wa 15 kwa viongozi na marais wa nchi ya  harakati huko Sharm El. -Sheikh mnamo kipindi cha kuanzia tarehe 11 hadi 16 Julai 2009. Mkutano huu unazingatiwa kuwa hatua  wa kipekee  katika  mwendo wa  harakati ya Nchi Zisizofungamana na Siasa wa upande wowote katika karne ya ishirini na moja, kama ilivyokuwa mkutano wa Kairo mnamo mwaka 1964 ; wakati  harakati ya ukombozi wa kitaifa ilikuwa kung'rika kwa hali ya juu   ulimwenguni , mkutano huu wa kilele ulikuwa hatua wa kipekee  katika historia ya  harakati isiyofungamana na Upande Wowote, ambapo  ulihamisha harakati hiyo kutoka kwa mfumo wa mfumo wa kisiasa hadi awamu ya maelezo ya kina ,  kushughulikiaji wa kina kwa maswala, na ilianzisha  mchakato wa kupanga maswala kwenye ajenda kulingana na aina yake, jambo ambalo limekuwa  la  kuiga, au sehemu maalum katika taarifa zijazo  za mwisho  za harakati.


Utendaji ulio na kifani wa misri wakati wa uongozi wake kwa harakati ya isiyofungamana na Siasa wa  upande wowote , ulichangia kufanikisha shughuli za  harakati hiyo mnamo kipindi kilichopita, na kuwezesha harakati hiyo kuzungumza kwa sauti moja na kuitikia kadiri itakavyo kwa  maendeleo yoyote yanayoweza kutokea katika uwanja wa kimataifa.

 Misri ,tangu kushika kiti cha Uongozi wa mkutano wa 15 wa harakati ya kutofungamana na Siasa za upande wowote,  imeendeleza mafanikio yaliyokufanywa na  viongozi waliopita  wa harakati hiyo ili kuimarisha nafasi yake katika ngazi ya kimataifa haswa  katika mfumo wa Umoja wa Mataifa. vilevile , imeendelea kufanya juhudi na kuratibu na nchi zote  wanachama ili kukamilisha kwa uaminifu utekelezaji wa Mpango  wa Sharm El-Sheikh hadi Mkutano  wa kilele ujao  nchini Iran.

Nyaraka zilizotolewa na Mkutano wa Sharm El-Sheikh zilisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya Kusini na Kusini kwa upande mmoja, na kwa upande mwingine,  kati yake na nchi zilizoendelea kiviwanda za Kaskazini , na kutahadharisha  baadhi ya nchi  za kiviwanda  kuchukua maamuzi ya upande mmoja  katika pande za  uchumi, fedha na biashara ambazo zingeweza kuwa na athari mbaya mno kwa nchi zinazoendelea, pamoja na umuhimu wa Ushirikiano kati ya Kundi la 77 na harakati isiyofungamana na Siasa ya upande wowote , ambazo zinapishana katika malengo na Uchama; na Kundi la 15, ambalo lilitokana na harakati isiyofungamana na Siasa ya upande wowote  katikati ya miaka ya 1980 mnamo karne ya ishirini  na kwa kawaida hufanya mikutano yake  pembeni mwa  makongamano ya harakati hiyo .

Wakati wa uongozi wa Misri kwa harakati hiyo , imeshapitishwa uchama wa Azerbaijan na Visiwa vya Fiji  pia kupitishwa kwa "tangazo la Bali" kwa harakati ya kutofungamana kwa upande wowote  kwa kuadhimisha  miaka hamsini tangu kuanzishwa kwa harakati hiyo,  ambalo limeainisha malengo na hatua za msingi  za kukabiliana na machangamoto ya kisasa, na inaainisha  maoni ya wanachama wa harakati  hiyo juu ya  masuala  na machangamoto  ya kimataifa   wakati wa miaka ijayo.

Rais wa zamani Mohamed Morsi alishiriki katika Mkutano wa 16 wa harakati  ya  kutofungamana kwa upande wowote, ambao ulikaribishwa na mji mkuu wa Iran, Tehran, wakati wa kipindi cha kuanzia tarehe 30-31 Agosti 2012 , ambapo alihamisha uongozi wa mkutano huo kutoka Misri kuelekea Iran. 

Ulimwengu na Mashariki ya Kati ulishuhudia matukio muhimu kati ya uongozi wa Misri kwa  harakati katika mkutano wa kilele wa Sharm el-Sheikh mnamo 2009 , na mkutano wa kilele wa Iran mnamo Agosti 2021 , kuanzia na janga la kifedha ulimwenguni lililozuka katika Marekani na  liliongezeka wakati wa  urais wa Obama, kisha matukio ya mapinduzi ya kiarabu yakaendelea, kuanzia Tunisia na kupita Misri , Libya, Yemen na Syria, kujitenga kwa Sudan Kusini, kuondoka kwa majeshi ya Marekani kutoka Iraq, hata ikiwa imebaki chini ya  udhabiti wa kijeshi na kisiasa wa  Marekani. na  imeongezeka  udhibiti wa Iran ndani yake, na kuongezeka kwa vita vya kidiplomasia, vitisho, kuwekewa vikwazo na kususia Iran kwa sababu ya faili yake ya nyuklia na kuituhumu kwa kufanya kazi  ili kutengeneza silaha za nyuklia.  kutokana na hilo  , umuhimu wa jukumu la harakati hiyo  mbele ya maendeleo hayo muhimu limeonekana wazi  katika uwanja wa kimataifa .

Mnamo Mei 4 , 2020, Rais Abdel Fattah El-Sisi alishiriki katika mkutano wa kilele wa harakati ya kutofungamana kwa upande wowote, ambao ulifanyika pamoja na anwani  ya "Tuko pamoja  katika Kukabilianana na  Janga la virusi vya Corona",  na hilo kwa kushirikisha  marais  kadhaa wa nchi na wanachama wa serikali ya harakati hiyo  , inayoongozwa na Rais Ilham Aliyev, Rais wa Jamhuri ya Azerbaijan na Rais wa sasa wa Harakati hiyo, pamoja na Rais wa kikao cha 74 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa , Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika, na Makamu wa Rais wa Tume ya Ulaya. Mkutano huo umekuja kwa lengo la kujadili na kuratibu kati ya nchi wanachama katika  harakati ya kutofungamana kwa upande wowote kuhusu athari za kuenea kwa janga la Corona, na kujadili njia za kukabiliana na janga hili katika nyanja zake zote za kiafya, kijamii na kiuchumi.

 Rais El-sisi - Katika hotuba yake wakati wa mkutano huo -   alisisitiza umuhimu wa ushirikiano  na mshikamano wa kimataifa  kwa ajili ya jibu la maana na la haraka kwa janga la Corona, haswa kwa kufanya kazi ili kuhakikisha upatikanaji wa vifaa muhimu vya matibabu na kinga vinavyohitajika , kuongeza juhudi za utafiti wa kisayansi  ili kuboresha dawa na chanjo ya virusi vya Corona, na juhudi za kimataifa za kusaidia nchi zinazoendelea na kutoa vifurushi vya kichocheo kwa uchumi wao, na kupunguza athari za janga hilo kwa usalama wa chakula Duniani.


vilevile ,Rais  amesisitiza kuwa, harakati ya kutofungamana kwa upande wowote inapaswa kuchukua  jukumu la msingi katika suala hili,  na hilo wakati wa  Misri ni miongoni mwa nchi zilizoanzisha harakati hiyo,  aidha kutokana na  kwamba inazingatiwa ni mfumo muhimu na mpana wa kuratibu misimamo ya nchi zinazoendelea kuhusu masuala mbalimbali katika ajenda ya mfumo wa kimataifa.

Na mnamo Oktoba mwaka huo huo, pembeni mwa  kikao cha 75 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, mkutano wa mawaziri wa  harakati ya  kutofungamana kwa upande wowote ulifanyika kwa ushiriki wa Waziri wa Mambo ya nje Sameh Shoukry kupitia mawasiliano ya kuona, ambapo Shoukry alisisitiza   kipaumbele cha hali ya juu ambacho Misri inakiangalia katika harakati hiyo kwa kuwa   ni mfumo muhimu ili kuratibu misimamo ya nchi zinazoendelea juu ya masuala  mbalimbali yanatolewa katika ajenda ya mfumo wa kimataifa ,  Akiashiria umuhimu wa   kushikamana kwa juhudi za  wanachama wake kwa ajili ya kurejesha imani katika njia za kufanya kazi  za pande nyingi na kukabiliana na  mfumo  wa siasa wa kuvutia  katika mfumo wa kimataifa ili kuweza kukabiliana na changamoto nyingi zinazoukabili ulimwengu wetu hivi sasa .

Waziri Shoukry pia alisisitiza umuhimu wa juhudi za pamoja za harakati ili kupambana na ugaidi na kukomesha vyanzo vyake, kuanzisha eneo lisilo na silaha za maangamizi katika Mashariki ya Kati, na kutunga kanuni za kusimamia mtandao na kudumisha usalama wa Sebrania . Vile vile,  amezungumzia msimamo thabiti wa Misri wa kuunga mkono kipaumbele cha masuluhisho ya kisiasa kwa mizozo ya Libya, Syria na Yemen,  pamoja na  haja ya kutafuta suluhisho la haki na la kina la suala muhimu la Palestina kwa mujibu wa maazimio ya uhalali wa kimataifa , jambo linalotekeleza matumaini halali ya watu wa Palestina ya kukomesha Ukoloni huo na kuanzisha nchi yao huru na mji mkuu wake ni Jerusalem Mashariki.

mnamo Juni 4, 2021, Balozi Dkt. Ahmed Ehab Gamal El-Din, mwakilishi wa kudumu wa Misri kwenye Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya kimataifa mjini Geneva, alishiriki katika mkutano wa Mawaziri wa nchi za harakati ya kutofungamana kwa upande wowote, unaofanyika  pembezoni mwa kikao cha 109 cha Mkutano wa Kimataifa .  Balozi Gamal El-Din - katika hotuba yake - alisisitiza kutilia maanani mwa Misri kwa   harakati ya kutofungamana kwa upande wowote  kwa kuwa  mmoja wa waanzilishi wake, akisisitiza jukumu lake muhimu katika mfumo wa pande nyingi na katika kuimarisha ushirikiano kati ya nchi zinazoendelea ili kufikia mustakabali bora kwa watu wetu. aidha ,Balozi Gamal El-Din aligusia hatua zilizochukuliwa na Misri ili kupunguza athari za kiuchumi na kijamii za janga hili kwa kupitisha sera za fedha  ili kuboresha uchumi Kutoa kiwango cha faida cha upendeleo  kwa mikopo, kuchelewesha faida za kodi na mikopo, kuimarisha mfumo wa ulinzi ya kijamii, taratibu za ukaguzi wa wafanyikazi, utoaji wa posho kwa ajira wasiodumu, ambapo wanawake wanawakilisha 40%, kufadhili miradi ya wanawake, kuzindua programu za elimu ili kuwaunganisha katika soko la ajira, na kutoa huduma za mapumziko  kwa  wajawazito Na kutunza watoto na wanawake wenye ulemavu.

Mnamo Agosti 22, 2021, Balozi Sameh Shoukry, Waziri wa Mambo ya Nje, alizungumzia Harakati ya kutofungamana kwa upande wowote, upanuzi wake, kujiunga na nchi zinazoendelea, na kufuatilia kanuni za nchi waanzilishi, akisema kwamba ilifika uwiano na utulivu katika mahusiano ya kigeni, wakati uliokuwa na mvutano, na kudhibitisha upande moja  kwa  upande mwingine,pia ilifanya kazi  ili kufikia mahusiano ya usawa na kukidhi matarajio ya raia wanaoendelea kwa utulivu na maendeleo. Shoukry aliongeza, wakati wa hotuba yake katika mkutano na waandishi wa habari unaofanyika sasa hivi na mwenzake wa Serbia, Nikola Sekolavić, kwamba miaka iliyopita ilishuhudia mivutano na machangamoto mengi ambayo yaliathiri vibaya  juu ya uwezo wa  Harakati ya kutofungamana  kutofikia malengo ambayo ilianzishwa kwa ajili yake . Shoukry aliomba kuwepo shughuli  zaidi kati ya wanachama wa harakati hiyo, kuunda mipango kwa mustakabali, kuainisha machangamoto na kufikia hatua ya kuafikiana kuhusu jinsi ya kusonga mbele na harakati hiyo, kwa njia  itakayotekeleza maslahi ya wanachama wake. Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri amesisitiza kuwa Misri inawajibika kuratibu, na inategemea mshikamano kati ya nchi za harakati hiyo na mashirika mengi ya kimataifa ili kuunda misimamo ya pamoja, na akiongeza kusema kwamba: "Wakati Harakati ya kutofungamana kwa upande wowote  inapozungumza kwa sauti moja, ni sauti yenye ushawishi na ufanisi ambayo inapitishwa."

Misri inaona kwamba  Harakati ya kutofungamana  kwa upande wowote inazingatiwa mfumo muhimu na mpana zaidi wa kuratibu misimamo ya nchi zinazoendelea kuhusu masuala mbalimbali ya kisiasa, kiuchumi na kijamii katika ajenda ya Umoja wa Mataifa, na kuunga mkono njia za kazi  za pamoja za pande nyingi ili  kukabiliana na sera za upande mmoja na za upande mmoja, ambazo ni mojawapo ya machangamoto makuu yanayokabilina nchi zinazoendelea, ambazo nyingi ni wanachama katika Harakati hiyo .
Misri inatilia maanani na  harakati hiyo na haja ya kuihifadhi kutokana na umuhimu wake mkubwa wa kikanda na kimataifa, kwani  inajumuisha karibu theluthi mbili ya nchi wanachama katika Umoja wa Mataifa ulimwenguni,  kwa hiyo inazingatiwa kundi kubwa la upigaji kura, na  inapaswa kufanya kazi ili kuimarisha mahusiano kati ya nchi zake ili kutetea maslahi yake na maslahi ya raia wake.

 inazingatiwa Mojawapo ya mihimili mikuu inayoegemezwa juu yake msimamo wa Misri juu ya  harakati ya kutofungamana na Siasa za Upande Wowote ambapo,  harakati hiyo endapo ilianzishwa chini ya mfumo wa kimataifa wa pande mbili, basi tofauti ya mazingira hayo inalazimisha kuendeleza zana za harakati hiyo, jambo ambalo linaipa uwezekano wa kuchangia - kupitia misimamo chanya na ya kweli inayokubaliwa  na nchi zake zote- Kuathiri mwendo wa  mwingiliano wa kimataifa.

Misri inaamini kuwa, kile kinachoshuhudiwa  katika uwanja wa kimataifa hivi karibuni katika suala la kuvunjwa kwa mihimili na misingi mikuu ambayo  Harakati ya kutofungamana kwa upande wowote   iliegemezwa ni jambo la kutia wasiwasi haswa lile  linalohusiana na kutoingilia katika masuala ya ndani ya nchi, kuheshimu hadhi yake , utulivu wake, na uhuru wa uamuzi wake, na kutotosheka kwa mamlaka ya kitaifa na umoja wa kikanda ili kuzuia Kuingilia mambo ya ndani ya nchi, badala yake, mambo ya ndani yenyewe yamekuwa kisingizio  kwa wale wanaotaka kulazimisha udhibiti wao juu ya wengine, na haya yote ni machangamoto makubwa ambayo yanayowajibisha  kuendelea kwa harakati pamoja na kuijenga upya na kukuza uwezo wake.
Nyaraka za harakati hiyo na  mwendo wake zinathibitisha nafasi ya kihistoria iliyotekeleza - na Misri inatekeleza - katika kuendeleza harakati na kuingiza roho mpya katika mwili wake.  na jukumu imara  la kimisri  imechangia katika kuanzisha na kuunda harakati ya kutofungamana na  siasa za upande wowote   pamoja na umuhimu wake wa ustaarabu na kisiasa ambao ni msingi unaozinatiwa na misri ili   Kuunga m mwendo wa  harakati hiyo katika siku zijazo kwa kuongeza juhudi zake za pamoja na nchi nyingi zinazofanya juu chini ili kuunga mkono harakati  kwa lengo la kuendeleza malengo na mbinu zake, na kuifanya iwe na ufanisi zaidi  kwa lile linalohusiana na kukabiliana na mabadiliko makubwa yanayotukia katika uwanja wa kimataifa kisiasa, kiuchumi, na kiutamaduni, hasa baada ya harakati hiyo ilibadilishwa kutoka chombo kinachojumuisha  nchi 25  Katika mkutano  wa kilele wake wa kwanza ,  kwa kuwa chombo kikubwa ambacho kwa sasa kinajumuisha nchi 118 za mabara ya Afrika, Asia, Ulaya, na Amerika ya Kusini.

 Misri   kwa  ushiriki wake wa ufanisi katika mikutano ya Harakati ya kutofungamana kwa upande wowote - tangu kuanzishwa kwa Harakati hiyo -  inathibitisha mwingiliano wake wa endelevu na jukumu la uongozi lake, sio tu   katika  kanda yake lakini pia katika ngazi ya kimataifa katika kuonesha masuala ya nchi zinazoendelea ili ziweze kupata  haki yake  ya kisiasa na ya  kimaendeleo katika nyanja ya kimataifa kutokana na imani yake kwa umuhimu wa kuimarisha kazi ya pamoja ya pande kadha kimataifa kupitia kuunga mkono wa Umoja wa Mataifa, mashirika na vyombo vyake, vinavyoongozwa na Baraza Kuu, kurekebisha na kuunda upya Baraza la Usalama la Umoja wa kimataifa kwa lengo la kulazimisha nchi wanachama kwa maamuzi yao, na sio kuzisukuma nchi hizi ili  kufanya kazi nje ya mfumo wa kimataifa na mbali na mfumo wa uhalali wa kimataifa.