Jukumu tulilokabidhiwa ni kubwa na kuu
Imefasiriwa na / Alaa Zaki El Ashry
Enyi Wananchi:
Kwa jina la Rais kiongozi, ninazungumza nanyi: Wote hawa wenye furaha na shangwe, na mbele ya heshima na ukaribisho uliozunguka shingo yangu, namshukuru Mwenyezi kwa kunipa nafasi ya kuzungumza nanyi.
Jukumu tulilokabidhiwa ni hatari na kubwa, ambapo ndio uaminifu ambao... Juhudi kubwa na majukumu makubwa yanayotukabili sasa yanaonekana kwangu kuwa mepesi baada ya kuona ile hisia kubwa inayotiririka ya uzalendo na shauku, jambo hilo lilinifanya nihisi kuwa matumaini makubwa yanayonijia kifuani mwangu ni mwangwi wa ukarimu wa kile unachohisi, na kuwa mizigo tunayobeba si chochote ila wajibu uliowekwa na uzalendo na ushujaa wako, na Misri yenye nafasi juu katika historia ina heshima kubwa na nafasi tukufu.
Enyi Wananchi:
Tunakaribia kipindi kigumu katika historia ya kisasa ya Misri, na sasa ulimwengu mzima unatutazama na tumerejesha imani yake kwetu katika mapinduzi yetu matakatifu, ambayo majaliwa ya Mwenyezi Mungu yalichukua, kuwafukuza wasaliti kutoka kwao, na kuyawezesha kuhakikisha, katika hatua zake za kimantiki, uongozi wa raia hawa wakuu.
Enyi Wananchi:
Mapinduzi yetu yalitokana na nyoyo zilizochoshwa na wale waliokuwa kuongoza watu hao, wakitoa damu zao na kutumia juhudi zao ili kuhakikisha matamanio na matakwa yao, na juu yao mfalme mzembe aliyezembea juu ya hirizi za dunia na mali zake, na pembeni yake palikuwa na mtu asiye na nia njema akimuomba chochote anachotaka, huko akiweka hofu kuwa hakuulizwa alichofanya.
Kuanzia hapa, mapinduzi yetu yalikuwa ni ghadhabu kuu na mwangwi wa hisia za raia wengi, hivyo mfalme akaondolewa, rushwa ikaondolewa, ukabaila ukaondolewa, vyama viliondolewa, wananchi wakakaa kujiweka katiba yao, na mioyo ilifunguliwa hadi baraza la wahariri lilipoundwa na nguvu za watu ilihamasishwa ndani ya wigo wa kauli mbiu yake ya muungano, utaratibu na kazi.
Enyi Wananchi:
Mapinduzi haya, yakiwa yameinua kichwa chake, hayatayapinda tena, na uendeleaji wa kuwepo kwa ukoloni na kuwepo kwa mapinduzi ni jambo lisilo la kawaida ambalo halijaidhinishwa na desturi ya mapinduzi wala mantiki yake yenye nguvu ya kutenganisha.
Enyi Wananchi:
Tangu tutwikwe mzigo, tumekuwa tukihangaika ili kudhoofisha nguzo za uvamizi, ambapo katika kusini, vita viliisha kwa kujitawala, lakini huku kaskazini hatutajisifu kama walivyokuwa wakisema - kwa njia ya mazungumzo-, lakini badala yake tunasema jambo moja: Ondokeni kutoka nchi yetu.
Enyi Wananchi:
Ni wana wa Nile tu watakaoulinda mfereji huo, na hatutaridhika nafsi zetu isipokuwa askari wa mwisho wa kigeni aondoke kutoka ardhi yetu nzuri.
Enyi Wananchi:
Lakini tunasema jambo moja tu: Ondokeni kutoka nchi yetu, ni wana wa Nile tu watakaoulinda mfereji huo, na hatutaridhika nafsi zetu isipokuwa askari wa mwisho wa kigeni aondoke kutoka ardhi yetu nzuri, ambapo hatutaafikiana katika haki ya nchi yetu, wala hatutaridhika badili ya uhuru wetu.
Hotuba ya Al-Bakbashi Gamal Abdel Nasser kwa niaba ya Meja Jenerali Muhammad Naguib katika jengo la Kurugenzi ya Beni Suef mbele ya hadharani waliokusanyika hapo.
Mnamo Machi 27, 1953.